ZIFAHAMU TABIA ZA WAJASIRIA MALI WANAOFANIKIWA


Image result for entrepreneurs

Mjasiria Mali ni nani
            Ni mwanzilishi mmbunifu mtu mwenye wazo na mtekeleaji wa mawazo ya kibiashara,ni mtu ambaye anauwezo wa kuona fursa nakuamua kuzifanyia kazi zile fursa kwa ajili ya manufaa chanya iwe katika sekta ya kilimo,usafiri,uuzaji  bidhaa au utaalamu na kuweza kutengeneza faida kupitia shughuli hiyo
1. Kuona fursa/Maono/Mawazo(Visualization)
                Mjasiria mali yeyote hua na uwezo wa kuona fursa kabla hata ya watu wengine kuweza kuziona na ni watu walio namaono ya mbali na kujua vitu gani vitahitajika baada ya mda Fulani hivyo wao mawazo yao hufurika fursa mbalimbali na kuchagua kitu kipi wakifanye na kukigeuza kua fedha.

2.Hufurahia kufanya vitu wavipendavyo
                Wajasiria mali   vyema na watewengi hupenda kufaya vitu viwapavyo furaha na ndio maanda hufanikiwa kwani katika kufanya kazi kwao hua ni njia mojawapo ya kufurahia maisha hivyo hua na mawazo ya kibiashara yawafurahishayo na ambayo hupokelewa vyema na wateja wao.
  
3.Wanauthubutu
Wajasiria mali na watu walio na uthubutu ambao hupambana na uoga wao na kufanya vitu wavitakavyo hiyo huhusisha kupoteza fedha katika mawazo wayaaminiyo na pia huhusisha uwezo wao wa kuamua na kuaznisha kitukatika mazingira hata yasiyo rafiki na hata kwa mitaji midogo.

4.Wanafanya kazi kwa bidii
                Wajasiria mali wanaofanikiwa hua na tabia ya kufanya kazi kwa bidii kama ni kutoa huduma kama ni kuuza bidhaa huhakikisha mteja hasikitiki kwa sababu ya wao kushindwa kukamilisha kazi au kata huduma kwa mda.
5.Ubunifu
                Wajasiria mali wanaofanikiwa siku zote hua wabunifu na watu wa kujifunza vitu vipya ili kuweza kutoa huduma bora au bidhaa bora na siku zote kujiweka katika chaguo bora katika jamii wanayofanya kazi.
6.Kupambana na uoga/hawaogopi kujaribu
                Wajasiria mali na watu wanaoamua kuushinda uoga ,kutojari kukataliwa ila huogopa kupoteza nafasi kwa kutokujaribu kabisa pia ni wapambanaji katika mawazo wanayoyaamini na kuyafanyia kazi kwa kupambana na vikwazo vyovyote vinavyoweza kujitokeza.
7.Hawajari Mitazamo/Hawaogopi kua tofauti
                Wjasiriamali wanaofanikiwa hutengeneza dunia yao wenyewe ambapo huishi kwa kufuata taratibu zao na sio mitazamo ya watu wengine wanavyotaka waishi mfano mjasiria mali anaweza kua kamaliza chuo ambapo inategemewa anatakiwa kuvaa tai au suti na kuonekana akienda kufanya kazi sehemu Fulani wao huweza kuamua kuvaa buti na kwenda shamba ilimradi anajua manufaa yake baada ya mda Fulani ambayo huweza kua makubwa kuliko yule anayeonekana bora akienda kufanya kazi kwa mtu.
8.Ni watendaji si wafikiriaji tu
                Wajasiriamali wanaofanikiwa hawa ni watu ambao wazo ikiwajia na wakilichanganua na kuona manufaa yake huamka na kwenda kulifanyia kazi si kuendelea kufikiria sana jinsi gani wazo litashindikana hawa ni watendeaji wa mawazo.
9.Wanajiamini.
                Wajasiriaa mali wanaofanikiwa ni watu wanojiamini kwani siku zote wao hua watu wa tofauti katika jamii na hufikiri vitu ambavyo jamii huona haviwezekani hivyo husimamia mawazo yao na hata mwisho kuweza kuthibitisha mawazo yao kwa jamii nayo kuweza kuwaamini kua inawezekana.
10.Wanamawazo chanya
                Wajasiriamali wanaofanikiwa hutawaliwa na mawazo chanya Zaidi na sio hasi na hiyo ndio siraha kubwa walio nayo kwani huchambua mambo kabla ya kuyafanya na kwa sababu wao huchukua risk/kujaribu hiyo huwafanya wao wawaze chanya ili kufikia malengo yao kwani mtu mwenye mawazo hasi hawezi kupiga hatua yoyote kwani anauhakika wa kushindwa tayari.
11.Wavumilivu.
                Wajasiria mali wanofanikiwa ni watu wenye uvumilivu wa hali ya juu ukiangalia mianzo ya bishara mbalimbali ni ya kukatisha tamma na ni wachache ambao huamini kufika kwake ila wao hupambana wakitegemea mema na hiyo ndio huwafanya wao pekee kusimama ingali wengine hushia njiani na biahsara zao kufa.
12.Wanatabiaa za uongozi/waanzilishi.
                Wajasiriamali wanofanikiwa wana tabia za uongozi ambazo ni kua na maono/vision pia utendaji wa vitendo kuhakikisha kufikia ile vision sio watu waelekezaji ni waelekezaji watendaji wanaotangulia mbele hivyo wao huwa na uwezo wa kujua vitu wanavyotaka vifanyike na huwa wataalamu mara nyingi kuliko wanaoongozwa kwani wao ndio wenye mawazo na hupokea mawazo/au ushauri na kujifunza.
13.Wanaadabu/Kuheshimu fedha
                Wajasiriamali wanaofanilkiwa hua na heshima kubwa ya kila wanachopata kama fedha si watu wafujaji wa hovyo wa fedha hiyo huwasaidia kupata nafasi ya kusonga mbele na kuweza kupanua na kukuaza biashara zao.
14. Wananjaa ya kutimiza malengo
                Wajasiriamali wanofanikiwa wananjaa kubwa ya kutimiza malengo yao si watu ambao wanataka kitu Fulani na kukiacha wakiamua jambo hulisimamia mpaka kufanikiwa kwake.
15.Hawatabiriki
                Wajasiria mali ni watu usioweza kuwatabiri wanafikiri nini katika wakati huu kwani vichwa vyao mda wote hua vinakua katika kufikiria tu na kubuni vitu vipya unaweza kunakili wazo hili na wakaibua wazo jipya hivyo mawazo yao ni mawazo endelevu.
16.Hawaishi kwa maonyesho wanajali kazi zao
                Wajasiriamali wanaofanikiwa wo huishi maisha ya kipekee hawafanyi maigizo katika maisha labda kufanya maigizo ni moja ya matangazo ya biashaa yao ila huamua kufanya vitu vilivyo na faida kwao.
18.Kujenga uamninifu
                Huamua kujenga uaminifu katika jamii inayowazunguka au watu wanaofanya nao biashara ili kutengeneza mazingira yao ya kudumu katika bishara.


Zilizoorodheshwa ni baadhi ya tabia muhimu kiutafiti ambazo zinapatikana kwa wajasiria mali wengi waliofanikiwa.


Imeandikwa na by:Stanley Mkolangunzi

Blogger:biznessstartupsecrets.blogspot.com

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Faida za kuanza na mtaji mdogo katika biashara

S&T HANDCRAFTED FASHIONS AND TOURISM