Faida za kuanza na mtaji mdogo katika biashara

Faida za kuanza na mtaji mdogo katika biashara 

Watu wengi ni wajasiriamali wanaotamani  kuanza bishara nao wana mawazo mazuri ya kuweza kuanzisha biashara ila hujikuta wamekwama kwa tatitzo la kukosa mitaji kwa ajili ya kuanzisha biashara au kuyafanyia kazi mawazo yao walionayo wanayoamini yanaweza kuwatoa toka sehemu moja kiuchumi hadi sehemu nyingine.Lakini katika msisitizo wangu kwa wote mnaosoma Makala zangu usiogope kwa kua na mtaji mdogo na kutaka mpaka uwe na mtaji mkubwa ili uanze kufanya biashaara ila anza tu .na Kama mtaji unao mdogo kabisa lakini unakuwezesha kuanza usisubiri kumiliki mamilioni ili kuanza kutendea wazo lako .
Faida za kuanzisha biashara ukiwa na mtaji mdogo
1.Unapata nafasi ya kuwajua wateja wako.
            Kwa kuanza na mtaji mdogo unapata nafasi ya kuwajua wapi ni wateja wako unajua umri wao,kipato chao ,tabia zao,tamaduni zao hivyo huo ni utafiti ambao unaufanya kwa kutumia mtaji mdogo huku unatengeneza faida yako kupitia biashara ndogo.
2.Unajifunza jinsi ya kutumia vyema rasilimali ulizonazo
            Unajifunza matumizi bora ya rasilimali ulizonazo kwani katika kipindi hicho ukiwa umeamua na unania ya kua mjasiriamali mkubwa utajitahidi kutumia mbinu mbalimbali za kuhakikisha wateja wako wanafurahi utajifunza mbinu mbalimbali za kupata bidhaa na mbinu mbalimbali za kuhakikisha rasilimali ndogo zinatoa huduma bora kwa wateja mfano unatoa hela kidogo kwa supplier wako na kumwomba aje achukue baada ya mda ili ukiuza ile fedha yake umlipe hivyo unatengeneza faida yako na supplier unamlipa na mteja wako kafurahi lakini kwa robo ya mtaji uliohitaji kua nao kufanya biashara hiyo
3.Unapata nafasi ya kukuza ndoto yako na kufikiri Zaidi
            Mtaji mdogo unapata nafasi ya kufikiri zaidi ni vitu gani unatakiwa viboresha lakini pia unapata fursa ya kuona mambo mbalimbali unayoweza yapanua ukipata mtaji na ndoto ya kipindi upo katika utendaji itakuwezesha wewe kuwa na mawazo mapana yaliyo kiutendaji na yenye asilimia kubwa ya mafanikio.

4.Unapata wateja utakao kua nao katika biashara
            Katika kipindi hiki unapata nafasi ya kua na wateja ambao watasimulia mwanzo wako ambao huweza kua nawe na kua mabalozi wa biashara yako jinsi inavyokua jinsi siku zinavokwenda.
           
5.Unajua nini wateja wako wanahitaji .
            Kipindi unabiahsara yako ukiwa na mtaji wako wateja wako katika eneo uliloamua kufanya biashara watakuja na maswali kuulizia huduma wanazozihitaji ni wewe kutumia maswali yao na kujua ni vitu gani unapaswa viongeza ukipata mtaji ili kukuza biashara yako.


6.Inakuepusha kupata hasara
            Inakuepusha kupata hasara isiyo ya msingi mfano wakati naanza biashara yangu niliweka blueband katika mtaa uliokua mpya na wateja wengi walikua ni wenyeji wasio na mazoea ya matumizi ya blueband hivyo niliweka boxi kadhaa ila kilichotokea bidhaa ile ilikaa mpaka iliexpire .kosa moja nilifanya research lakini haikujitosheleza lakini kwa bahati sababu nlikua na mtaji mdogo baadhi ya vitu nlivoshindwa kufanya wateja waliviitaji nlipopata fedha nkaviweka mwitikio wake ulikua mzuri sikuwahi kuweka bidhaa iliyoniharibikia nikapata hasara tena.
7.Unapata nafasi ya kuunda brand yako/Unajitangaza
            Kipindi ukiwa na mtaji mdogo unapata nafasi ya kujitangaza waweza kutambulisha kijiwe au unaanza kujulikana kidogo na taarifa husambaa sana hivyo kipindi umepata mtaji unakua umekwisha fahamika. Hivyo ni vizuri kama umeajiriwa na unategemea baada ya mda fulani utataka ujiajiri anza kujitambulisha hivyo hata kama una mtaji mdogo anza itakua na faida kubwa kwako hapo mbeleni.
8.Biahashara ya mtaji mdogo ni chambo
            Ukiwa na biashara hata kama ina mtaji mdogo na hujui utapata vii mtaji basi ile biashara yako ni chambo cha kukupatia mtaji mkubwa .mfano nilianza nikiwa na biashara ndogo kabisa lakini kwa bahati nzuri kuna benki waliita wakasema kama utahitaji mtaji tunaweza kukupa uongezee ili kubororesha biashara yako lakini hakuna atakayekuongezea kama hujaanza kutafuta.

Lengo kuu la Makala hii ni kukuambia kwamba usijali unakidogo kiasi gani anza kupitia hicho ulicho nacho na hatua ya kwanza utakayopiga itazalisha hatua ya pili ila ukikaa na kusubiri huwezi kuanza wala fika popote katika mapambano ya mafanikio au hasara unayoweza pata utapata mtaji wazo lako la biashara likiwa limekwisha mda wake sipendi useme ningejua ningeanza na fedha ile ndogo wakati unamuona aliyeanza na fedha kidogo .Musa aliulizwa umeshika nini mkononi wewe umeshika nini mkononi hivyo ulicho nacho kinatosha kukuvusha katika bahari ya umaskini au kukufanya ufurahie maisha yako kwa kutimiza ndoto zako .kama unataka kua consultant,engineer mwimbaji mchekeshaji,mwigizaji anzia hapo ulipo.
Imeandaliwa na
Stanley Mkolangunzi
Entrepreneur &Motivational speaker
Blog:biznesstartup secrets .blogspot.com
Youtube:Skills& Motivations TV


Comments

  1. Nawashukuru sana, leo naanza kwa kufuata ushauri wenu, nitaendelea kuwafuatilia na nitawapa muelekeo wa biashara yangu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Karibu tena tujifunze inawezekana kuishi ndoto yako mjuze na mwingine apae maarifa kupitia blog yetu

      Delete
  2. Hi,
    I having many kinds of knowledge from your blog.. keep sharing !if you want tax return services bangalore list of audit firms bangalore click on it

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

S&T HANDCRAFTED FASHIONS AND TOURISM

ZIFAHAMU TABIA ZA WAJASIRIA MALI WANAOFANIKIWA