Jinsi ya Kuongeza Mauzo kwa kuzingatia Fikra za mteja
JINSI YA KUONGEZA MAUZO
KWA KUZINGATIA FIKRA ZA MTEJA
Katika vitu
nimejifunza katika biashara na baada ya kufanya utafiti juu ya wateja wengi ni
kwamba mteja anapokuja katika biashara yako si kwamba anakuja kwa sababu sehemu
nyingine hakuna bidhaa kama hiyo ila ni kwamba kwako anapata bidhaa Zaidi ya
hivyo vitu anaweza pata sehemu nyingine.
Unapofanya
biashara ukiweza kujumuisha na hisia unaweza washawishi wateja wengi Zaidi kwani
hisia humfanya mtu kua mtumwa wake na hivyo kuna fursa ya kuongeza mauzo na mapato
kama utaweKa na bonus ya hisia katika bidhaa au huduma zako.
1.Mteja wa thamani
Kuna huduma
zinaitwa mteja wa thamani hii ni huduma wengi tumekutana nayo mfano katika
mabenki au katika huduma mbalimbali watu hua tayari kutoa fedha zao ilimradi
kwanza wapewe kipaumbele cha thamani hata kwa kuongezewa vitu vidogo sana
lakini wapo tayari kutoa fedha Zaidi kwa sababu wameitwa na wameonekana wa
thamani.
2.Hisia ya kwamba ni bei rahisi
Hiyo ni hisia
ambayo mteja anatengenezewa kwamba kununua katika utaratibu Fulani itamfanya
alipe kwa gharama ndogo Zaidi mfano ukilipa kifurushi cha mwaka unapata punguzo
la 20% na ukilipa kila mwezi itakua gharama 100% hivyo mteja akipata hiyo fikra
na hisia anaweza kua tayari kulipa kwa mwaka au jumla ili tu apate huo upendeleo wa punguzo la bei.
3.Hisia kwamba yeye ndio wa kwanza na
amepewa tofauti
Mashirika
mbalimbali wanatumia njia tofauti kuhakikisha kua wanatengeneza mfumo ambao
utawawezesha wateja kupata huduma ambayo itategemea matakwa ya mtu na mapenzi
ya mtu sio bidhaa ambayo kila mtu anayo.mfano kama unataka suti unashonewa kwa
kufata vipimo vyako na kama kuna kitu unataka kiongezeke unawekewa.na wamekua
wakitumia taarifa hivyo mteja anapofika wanachukua taarifa zako lakini pia kwa
kutumia teknolojia wanaweza kufatilia taarifa zako na kufanya utafiti juu yako
kwa mifumo inaitwa analytics kujua vitu unavyopenda,tabia na matumizi yako na
wafanyabiashara wengi wadogo kwa wakubwa wamekua wakifanya hivyo mfano kuna mtu
alikua anauza mitumba akachukua namba ya dada Fulani kila akifungua mitumba
mipya alimpigia simu yule dada na
kumwambia nimefungua kabla sijawaita watu wengine njoo uangalie wewe kwanza na
huyo dada alikua akienda lazima
anunue .
4.Hisia za uharaka katika upatikanaji wa
huduma au bidhaa na urahisi wa upatikanaji bidhaa
Mfanya biashara
akiweza kumpa mteja hisia kwamba akienda kwake atapata huduma haraka na kwa
urahisi bila usumbufu ana uwezo wa kuvutia wateja wengi Zaidi.mfano kumekua na
vilinganishi mbalimbali vinatumika kuangalia ni nchi gani unaweza kwenda
kufungua kampuni kwa urahisi katika Africa kuliko nchi nyingine na wapi ni
gharama rahisi hivyo mfanya biashara akiweza kutengeneza hisia hiyo pia na
kuweka mifumo inayomfanya huduma zake zipatikane kwa urahisi anaweza pata
wateja Zaidi mfano biashara kwa mtandao nk.
Imeandaliwa na :Stanley Mkolangunzi
ReplyDeleteVery Informative and creative contents. This concept is a good way to enhance the knowledge. thanks for sharing.
Continue to share your knowledge through articles like these, and keep posting more blogs.
And more Information Enterprise application for Construction