ZIFAHAMU FAIDA ZA KUA MJASIRIA MALI


Related image

Mjasiria Mali ni nani
            Ni mwanzilishi mmbunifu mtu mwenye wazo na mtekeleaji wa mawazo ya kibiashara,ni mtu ambaye anauwezo wa kuona fursa nakuamua kuzifanyia kazi zile fursa kwa ajili ya manufaa chanya iwe katika sekta ya kilimo,usafiri,uuzaji  bidhaa au utaalamu na kuweza kutengeneza faida kupitia shughuli hiyo
1. Unakua kiongozi wa maisha yako
            Unaapokua mjasiria mali unapata nafasi ya kua na maamuzi ya maisha yako na wapi unataka kwenda na wapi au kwa kiasi gani unaeza fikia kwa malengo yako ya kimaisha kwani ukiajiriwa utakua ukishi kwa mnyororo ulopangiwa na mjasiria mali aliyeanzisha hiyo kampuni unayoifanya kazi.
2. Uhuru
            Mjasiria mali anapata uhuru wa kufanya mambo yake na kupanga ratiba zake pia kuweza kufurahia maisha si kama muajiriwa ambaye mda wake unaendeshwa na mwajiri wake inakupa nafasi ya kushiriki mambo yako ya kijamii unapata nafasi ya kujaribu mambo mbalimbali katika maisha.
3. Kipato kisicho na kikomo
             Unaeza kujitengenezea kipato kisicho kikomo ni vile utavokua biashsara yako ikiongezeka ndivyo kipato kitavyoongezeka ambacho utakua na mamlaka ya kiasi gani unataka kujilipa
4.Uchaguzi wapi uishi
            Unapokua mjasiria mali unakua na muamuzi mmoja aliye rafiki yako ambaye ni mteja hivyo unauamuzi wa kuishi popote pale wateja wako walipo si vile kupelekwa sehemu mida mingine hupendi kua katika maeneo yale .
5.Uwezo wa kuzitumia fursa
            Unapokua mjasiria mali unapata nafasi ya kuweza kuzipata fursa kwa urahisi Zaidi ukilinganisha na ukiwa mwajiriwa ambaye mda wako unaendeshwa na vigumu kwenda kutumia fursa zinazopatikana katika mazingira na jamii.
6.Unakua wewe ndio Boss/nafasi ya kua mmiliki
            Unapokua mjasiria mali wewe ndiwe uliye na maamuzi juu yako na mshauri wako nimteja wako ambaye siku zote wapaswa muheshimu kwani ndiye anayekufanya uwe boss.

7.Nafasi ya kufanya kazi itayoishi vizazi
            Ukiwa mjasiria mali unaeza anzisha biashara au shughuli ambayo vizazi vitaweza kufaidi kupitia wewe na kukumbuka kwa kuwasaidia ,kutoa ajira na misaada kwani ukiwa mmiliki ni rahisi kukumbukwa kuliko ukiwa mfanyakazi ambaye anabadilishwa kwa vipindi tofauti kutegemeana na kampuni au shirika linavyoenda.
8.Kutengeneza ajira kwa watu
            Unapokua mjasiria mali unatengeneza ajira kwa watu wengine hivyo kwako inakupa nafasi ya kusaidia maisha ya watu wengine walio katika hali ngumu.
9.Unafanya kile kitu unakipendenda
            Unapokua mjasiria mali unapata nafasi ya kufanya shughuli unazofurahia kuzifanya katika maisha yako na pia unapata nafasi ya kua mfano wa kuwavutia wengine katika maisha kuanza kufanya vitu wavipendavyo.
10.Unapata nafasi ya kubadili dunia
            Njia pekee ya kuweza kufanya mabadiliko ya kitu Fulani ni wewe kusimama na kuanza kufanya kitu chako kitakachokua  na manufaa katika jamii yako yale uyapendayo hivyo unauwezo wa kusogeza huduma Fulani sehemu na kufanya maisha ya jamii ile kuboreka na kuleta mapinduzi chanya.
Faida nyingine
            Unapata nafasi ya kuishi ndoto zako unapata nafasi ya kuijaribu Imani yako unapata nafasi ya kufurahia kupitia mambo uyaaminio na kufurahia masiha katika namna ya kipekee na watu au timu yako utayoiunda.
 Hizi ni sababu zangu kumi kwa nini uwe mjasiria mali katika maisha yako naamini nimeamsha hulka na kukupa maana kwa nini uwe mjasiria mali.
Stanley Mkolangunzi-Blogger:Biznessstartupsecrets.blogspot.com
Phone                                    : +255 764-098564

Email                                     : smkolangunzi@yahoo.com

Comments

Popular posts from this blog

Faida za kuanza na mtaji mdogo katika biashara

S&T HANDCRAFTED FASHIONS AND TOURISM

ZIFAHAMU TABIA ZA WAJASIRIA MALI WANAOFANIKIWA